Sep 25, 2012

RAIS KIKWETE AKEMEA UPINZANI,,,,

KAULI YA RAIS KIKWETE KUHUSU WANAOSEMA CCM INAFIA MIKONONI MWAKE......


Rais Jakaya Kikwete
President Jakaya Kikwete ambae pia ni mwenyekiti wa CCM Taifa amewatoa wasiwasi wanachama wa CCM baada ya habari kusambazwa kwamba chama hicho kinakaribia kumfia, yani kinafia mikononi mwake kutokana na kushindwa kukiongoza.

Akiwa White house Dodoma amesema wanaoeneza hayo maneno ni wapinzani wa kisiasa ambapo amesisitiza kwamba uongozi wake hautasikiliza madai hayo na utaendelea kupitisha viongozi kulingana na sifa zinazohitajika.

Kuhusu baadhi ya wagombea kukatwa majina yao kwa madai ya upendeleo amesema hawajapitisha jina hata moja kama ilivyopendekezwa na mikoa na badala yake wanawapitisha wagombea kulingana na ujuzi, elimu na uzoefu ndani ya chama.

No comments:

Post a Comment