Apr 19, 2013

SEKESEKE MH! MKE AMSHUSHIA KIPIGO MUMEWE BAR,,,,,




Mwanamke mmoja ambaye jina lake halikuweza kufahamika mara moja, hivi karibuni alizua sekeseke la aina yake baada ya kumvaa mwanaume anayedaiwa ni mume wake na kumshushia kichapo.
Tukio hilo la aina yake lilitokea mwishoni mwa wiki iliyopita kwenye Baa ya Corner iliyopo Afrikasana, Sinza jijini Dar ambapo inadaiwa chanzo cha vurumai hilo ni mwanaume huyo kutoonekana nyumbani.

Chanzo chetu kilichokuwa eneo la tukio hilo kilitutonya kuwa, awali mwanamke huyo alitinga katika kiwanja hicho cha kujidai asubuhi na mapema huku akionekana kuangazaangaza huku na kule kabla ya kukutana na bwana wake huyo na kuanza kuzozana.
“Yule mwanamke alipofika hapa alionekana alikuja kishari na hata alivyokuwa akiongea na yule bwana wake tulibashiri kutokea kwa ugomvi.

No comments:

Post a Comment