Jul 30, 2012

WANAWAKE ACHENI KUWA MAGOLIKIPA..

CHOMA MAHINDI, KAANGA KARANGA DO SOMETHING BASI,,,,



Kujituma ni jambo zuri sana miongoni mwa binadamu, wapo watu hii leo ambao hulalamika ugumu wa maisha ilihali hawafanyi shughuli yeyote ya kujiingizia kipato au kujipatia ridhiki.


Wanawake wengi katika miji mikubwa hapa nchini wamekuwa ni watu wa kukaa majumbani tu iwapo wamekosa kazi za kuajiriwa maofisini jambo ambalo linapelekea kupachikwa majina mbalimbali ikiwapo lile la UGOLI KIPA.


Kwanini uitwe Goli kipa huku zipo shughuli mbalimbali ambazo wewe zinaweza kukupatia kipato na ukaweza ama kuendesha maisha yako na kujiepusha na vitendo vibaya au hata kujipatia fedha ndogo ndogo za mahitaji yako binafsi.


Daima kushinda majumbani kwa wanawake wengi wasio penda kujiajiri na kujishughulisha na vitu vidogo vidogo kama kuuza karanga, kuchoma mahindi, vitumbua na maandazi, husababisha wanawake hawa kuwa na majungu na mambo mengi ya Umbea. 



Baadhi yao wanasema kujishughulisha kunawafanya kujiepusha na makundi yanayoendekeza umbea mitaani na kusengenyana, lakini pia kuisaidia familia na wao wenyewe kuepuka kuwa omba omba hata kwa mafuta ya kujipaka.


Pichani ni mwanamke mkazi wa Jijini Arusha akijishughulisha na uuzaji wa Karanga, biashara ambayo inamuingizia kipato japokuwa ni kidogo lakini anaweza kumudu maisha yake na kuongeza pato la familia wakati baba amekwenda katika shughuli nyingine.

Biashara ya uchomaji Mahindi ni biashara ambayo imeshamiri katika maeneo mbalimbali ya nchi hususani jijini Dar es Salam na jijini Arusha. Hapa jijini Arusha asilimia kubwa ya wachoma mahindi ni wanawake.


Blog inachukua fursa hii kumtaka mwanamke yeyote ambaye ana uwezo wa kufanya kitu pale alipo na aanze sasa kufanya hivyo. Ipo dhana ya kusema Mwanamke akiwezeshwa anaweza lakini ukweli ni kuwa mwanamke akijituma anaweza hebu anza sasa na utaona matunda yake, na waala usitake mtaji wa kuanza duka la vipodozi au nguo kama jirani yako.

No comments:

Post a Comment