Sep 3, 2012

NIMERUDI DAR ILA SIO KUSAKA MWANAUME,,,

SIKU chache baada kukanyaga ardhi ya Bongo kutoka uhamishoni nchini Kenya, nyota wa muziki wa kizazi kipya Afrika mashariki Rehema Charamila amesema kuwa hajarejea nchini kusaka wanaume.
Akizungumza juzikati jijini Dar Ray C amefunguka kuwa hakuja Tanzania kutafuta Bwana wa Kuolewa nae kama watu wanavyovumisha mitaani isipokuwa amefanya hivyo kwa ajiri ya mapumziko na kazi pia.
"Unajua mimi niliamua kuhamia Kenya baada ya kuona kuwa ninsupport kubwa kwa Mashabiki wa huko kuliko hapa Tanzania hivyo nikaamua kwenda kuwapa kile wanachokipenda na pia kujaribu kukuza muziki wangu, katika kusibitisha hilo hivi karibuni natarajia kuachia ngoma yangu mpya amabayo nimeipa jina 'Moyo Waniuma' alisema Ray C.

No comments:

Post a Comment